Saturday 4 July 2009

Back to blogging!

pata hisotria fupi na picha za kijana alifanikiwa kuingia NBA
kutoka tanzania hashim thabit wakati huo akiwa mitaa ya sinza dar na baadhi ya vijana wa udsm outsiderz.

Saturday 11 August 2007

CCM London Chapter- Birmingham Mkutano!

Leo tarehe 11 Agosti 2007 CHAMA CHA MAPINDUZI tawi la London wamefanikiwa kufanya mkutano wao wa kwanza katika jiji la Birmingham!

Mkutano huo ambao ulianza saa 9 hivi mchana na kumalizika saa 12 jioni kama ulivyopangwa ulionekana kuwa na mafanikio makubwa. Tofauti na mikutano kadhaa ya tawi hili ambayo imeshafanyika jijini London na katika shina la Reading, mkutano huu ulionekana kuwa na idadi kubwa zaidi ya wanawake kitu ambacho kimekuwa ni changamoto kubwa, idadi ya akina mama/dada hao ilikuwa ni zaidi ya akina mama/dada kumi na mmoja!

Baada ya M/kiti wa muda wa Tawi Ndg. Maajar Sharrif kufungua mkutano huo na kutambulisha wajumbe wa muda wa tawi na wale viongozi wa muda wa shina la Reading, wajumbe wengine na wanachama wapya nao walijtambulisha na baadhi ya wajumbe toka Reading ambao waliambata na viongozi wao wa shina nao waliweza kujitambulisha pia. Mmoja wa wajumbe toka Reading ambaye alikuwa ameambata na ubavu wake, Bwana Alan Kalinga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tanzania Youth Sports Charity Organization (TYSCO) ametimiza ahadi yake ya kujitolea kompyuta mpya kwa ajili ya ofisi ya Tawi.

Naye Katibu wa muda wa tawi ndg. Richard Mpopo alisoma historia fupi ya tawi tangu kuanzishwa mwezi wa februari 2007 na mpaka kufikia siku ya leo, ambapo aliweza kufannunu kwa kina maendelo ya tawi kwa kilichofanyika kila mwezi kuanzia tawi lilipofunguliwa, vikao vilivyokwisha fanyika, kupatikana kwa ofisi, uzinduzi wa shina la la mji wa Reading na kutembelewa na wageni ambao ni viongozi wa CCM nchini Tanzania, pia alieza malengo makuu mawili ya tawi kwa sasa ambayo ni ;

1) Kuendelea Kuandikisha wanachama wapya na
2) Kujiandaa kwa uchaguzi wa viongozi wa kudumu wa Tawi hili.


Pia mkutano huu ulifanikisha kuchagua kamati ya muda ya wana-CCM Birmingham ambao wataendeleza shughuli za chama na hatimaye kuitisha uchaguzi watakpokuwa tayari kufikia idadi ya kuweza kuunda shina lao, ambapo wasema hatawachukua zaidi ya mwezi mmoja!

Zaidi ya hapo kuliwako na vitafunwa na picha ya pamoja baada ya M/kiti kuahirisha mkutano!

CRDB- Abroad/Tanzanite Account!

Hatimaye wateja wa CRDB ughaibuni hasa nchini Uingereza kuanza kunufaika na akaunti ya Tanzanite!

Wiki hii wawikilishi wa CRDB wametuma barua pepe kwa wateja wake walioko nchini Uingereza kwamba mipango imekamilika kwa wao kuweza kutuma fedha nyumbani kupitia "collective account" kwenye matawi ya banki ya Lloyds (TSB) nchini Uingereza.

Mteja wa CRDB mwenye akaunti ya Tanzanite ataruhusiwa ku-deposit paundi za kiingereza zisizozidi elfu moja (£1,000) kwa mwezi kwa gharama ya paundi moja (£1), kama mteja ata-deposit kiwango zaidi ya hicho kilichoweka kwa mwezi atalipa gharama ya puandi hamsini (£50) na kama akifanya hivyo zaidi ya mara moja akaunti yake itakuwa matatizoni.
wateja watatikiwa kutumia kitabu maalumu cha ku-deposit fedha hizo, vitabu hivyo kwa kila mteja vinapatikana kwa wawikilishi wa CRDB nchini Uingereza ambao ni ndugu Benard Chisumo wa Reading na Ndg. Patrick Kinemo wa Brighton. Pia kadi za baadhi ya wateja waliofungua akaunti zao wakiwa nchini Uingereza tangu mwezi wa februari mwaka huu wa 2007 zinapatikana kwa wawikilisha hawa.


kazi kwenu mlioko ughaibhuni.

"Fanya kazi kama mtumwa Ulaya Uishi kama Mfalme Afrika"

Thursday 26 July 2007

PANIC ATTACKS

Je umewahi kuusikia ugonjwa/hali hii? Kwa lugha ya Kiswahili nimeambia unaitwa UGONJWA WA WASIWASI! Labda wataalamu wanaweza kutusaidia!

Binasfi nimeufahamu rasmi ugonjwa/hali hii mwaka mmoja tu uliopita! Ni baada ya kuwa kupata maelezo kutoka marafiki wa karibu ambao baadhi yao wamekuwa wakisumbulia na hali hii kwa zaidi ya miaka sasa!

Daily Mirror Tuesday, July 24,2007

You`re just heading out the house when suddenly your heart is pounding, your throat`s tightening and you`re fighting for breath- welcome to the world of..
Panic attacks

THE SYMPTOMS

i) A choking sensation

ii) Feeling nauseous

iii) Your heart start racing

iv) A churning in your stomach

v) Experiencing hot or cold sweats

vi) Pains in your chest

vii) Hearing a ringing in your ears

viii)You start Hyperventilating

ix) A fear that you are going mad or having a heart attack

x) Feeling of impending doom

HOW TO COPE

i) Cognitive behavioural therapy (CBT) and other talking therapies can be very effective. This works by helping the sufferer to change long-held beliefs and behaviour. Speak to your GP about being referred.

ii) Anti-depressant medication helps some sufferers- a class of drugs called selective serotonin reuptake inhibitors (SSRIs) can help to reduce anxiety.

iii) Learning relaxation techniques such as yoga, meditation and hypnotherapy is also effective.

iv)Diet can make a difference, especailly cutting caffeine which increases anxiety.

Saturday 14 July 2007

The Lucky Child!

kuna imani kwamba namba saba(7) ni namba inayoambatana na bahati "nzuri". kama ambavyo wenzetu wazungu uamini kwamba tarehe 13 ya ijumaa (Friday 13th) ni siku mbaya!

Mtoto mwenye bahati alizaliwa Uingereza tarehe 7(saba), mwezi wa 7(saba), Mwaka huu wa 2007, katika wadi namba 7(saba), kitanda namba 7(saba), na mtoto wa 7(saba) katika famila yao, zaidi ya hayo baba yake ana umri wa miaka 3(7)(Saba) na hadithi hii imechapishwa kwenye ukurasa wa 7(saba) wa gazeti la The Mirror.

Pata habari kamili kupitia blogu hii kesho saa 7(saba) mchana!

The Lucky Number Seven!

Samehe 7(saba) mara 7(saba)0

The Hewden Auction



The Hewden Auction is the largest Euro Auction taking place kila mwaka ndani ya UK. Mnada huu uhudhuliwa na watu mbali mbali toka pande zote za dunia. Ni mnada maalum kwa vifaa hasa vya ujenzi (construction plants), pia unaweza kupata vifaa mbali kama generators, vifaa vya mechanics,magari(vans,trucks) na mengine mengi. Ukipenda kujua zaidi tembelea www.tsauction.co.uk



Tuesday 19 June 2007

Bongo Inavyoliwa na Wachache!




Soma habari hizi tatu tofauti kutoka vyanzo tofauti jaribu kupata picha kamili!






1)Ni kwamba tuna fedha sana au? (source: darhotwire)




Ghorofa mbili za Benki Kuu ya TZ zilizojengwa kwenye eneo la mita za mraba 40,000 zimelamba mshiko zaidi ya mara nne kama zingejengwa katika miji tajiri kama New York, London
na Tokyo
.Akimwaga takwimu hizo kwa machungu Kiongozi wa kambi ya upinzani na Waziri kivuli Wizara ya Fedha, Hamad Rashid Mohamed alisema kuwa hivi sasa gharama za kujenga mita moja ya mraba katika mataifa tajiri ni dola za Marekani -$2000.Lakini kwa gharama zilizotumika kujenga minara miwili ya BoT (40,000sq m), dola za Marekani -$8000 zilitumika kujenga mita moja ya mraba.Mwaka jana gharama za ujenzi zilitajwa kuwa dola za Marekani mil. $150 lakini kiasi hicho kimeshazidi sana na hivi sasa BoT inaendelea na ujenzi bila ya kutaja gharama halisi zilikofikia.Mh. Mohamed alisema kuwa hadi sasa majengo hayo hayajamalizika ingawaje yalishafunguliwa rasmi na Rais Mstaafu Benny Mkapa wa awamu ya tatu katika kilichoonekana kama kukurupuka.Hiki si kimeo cha kwanza kwani BoT inahusika na kashfa nyingine ya kutoa mshiko kwa kampuni ya Mwananchi Gold Project inayojihusisha na usafishaji wa dhahabu na nyingine ya dhahabu ya Meremeta.Ndani kwa ndani vilevile kuna vimeo vya upotevu wa fedha na hivi sasa wamesakwa wakaguzi kutoka nje ya nchi ili kuichambua Benki hiyo kubaini kiasi kamili kilichoyeyuka.Wakati yote haya yanaendelea nafasi ya Gavana wa Benki hiyo iko poa tu na hakuna anayesema juu ya lolote kama aachie ngazi au .............anyway si kasumba yetu.






2)Umaskini wetu unaletwa na viongozi - Anne Malecela 2007-06-20 08:47:31 Na Boniface Luhanga, Dodoma




Mbunge wa Same Mashariki (CCM), amesema watu waliopewa dhamana ya kuongoza nchi hii ndio wanaoimaliza kwa kuzidi kuitumbukiza katika janga la umaskini. Akiongea kwa uchungu bungeni jana, Mbunge huyo, Bi. Anne Kilango Malecela, aliwakemea vikali baadhi ya viongozi serikalini wenye dhamana ya kusaini mikataba kuwa waaminifu kwa kuweka maslahi na uzalendo mbele na kumuogopa Mungu, vinginevyo watalifikisha taifa mahali pabaya. Hali kadhalika, mbunge huyo amesema hakubaliani hata chembe na hatua ya serikali ya kupitisha moja kwa moja (fast tracking) bila ukaguzi bidhaa zote zinazoingizwa na wafanyabiashara ambao `eti` tayari wameainishwa kama wawajibikaji wazuri katika kulipa kodi. Bi. Malecela alitoa msimamo huo jana alipokuwa akichangia hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya serikali kwa mwaka ujao wa fedha (2007/08). Hotuba hiyo iliwasilishwa Bungeni Alhamisi iliyopita na Waziri wa Fedha, Bi. Zakia Meghji. Akielezea suala la mikataba, mbunge huyo alisema, anaamini kwamba Tanzania siyo maskini kiasi hicho lakini kinachochangia kuiangusha, ni mikataba mibovu inayosainiwa na baadhi ya viongozi wenye dhamana hiyo ambao hawazingatii uzalendo na maslahi yaTaifa. Kwa mujibu wa Bi. Malecela, Tanzania ni nchi ya tano barani Afrika kwa utajiri kutokana na kuwa na raslimali nyingi. Hata hivyo, alisema pamoja na hali hiyo, bado Tanzania inaonekana kuwa maskini na kwamba umaskini huu ni wa kujitakia kwani unachangiwa na viongozi wenye ubinafsi. `Kila anayesaini mkataba, amuogope Mwenyezi Mungu? Amtangulize Mungu wake mbele? Nchi hii si maskini kiasi hiki, ni tajiri na yenye raslimali nyingi ambayo inashika nafasi ya tano katika Bara la Afrika,` alisisitiza kwa uchungu. Alisema Rais Jakaya Kikwete, ameonekana kuwa amedhamiria kuitumikia kwa dhati nchi yake na ndio maana amekuwa akisema mara kwa mara kuwa anakerwa sana na umaskini wa Watanzania walio wengi, lakini baadhi ya watendaji, wanataka kumuangusha. Alitolea mfano wa Shirika la Ndege (ATC) ambalo aliwahi kulifanyia kazi, kwamba limefikishwa mahala liliko sasa ambako ni mahututi kutokana na mikataba hiyo isiyoangalia maslahi ya nchi yetu. Alimshauri Rais Kikwete kuwachukulia hatua kali watendaji wa namna hiyo bila kuwaonea huruma. `Ukimwangalia nyani akilia, anatia huruma kuliko hata mjane na ukitaka kumuua nyani anayekula mazao yako shambani, usimwangalie usoni maana utamuone huruma,` alisema akimaanisha kwamba, Rais Kikwete awachukulie hatua kali watendaji wabovu pasipo kuwaonea huruma. Aliwataka watendaji katika ngazi zote Rais Kikwete kutokana na jitihada zake na kila mmoja ahakikishe anatimiza wajibu wake. Kuhusu hatua ya serikali ya kupitisha moja kwa moja (fast tracking) bila ukaguzi bidhaa zote zinazoingizwa na wafanyabishara ambao tayari wameainishwa kama wawajibikaji wazuri katika kulipa kodi, Bi. Malecela alisema hakubaliani hata kidogo. Alisema anaamini kabisa kuwa kila mfanyabiashara awe mdogo ama mkubwa, hufanya biashara zake kwa kutaka kupata faida kubwa zaidi siku zote. Aliihoji serikali imenguanduaje uaminifu wa wafanyabiashara hao hata ikaamua kufikia hatua hiyo. `Tena mmewachagua wafanyabiashara watakaopitisha bidhaa zao bandarini bila kukaguliwa eti wameonyesha kuwajibika, hivi mmeingia mioyoni mwao lini (na kuona kwamba sasa wao ni sawa na malaika?),` Alihoji na kuongeza kamwe yeye hilo hakubaliani na kuitahadharisha serikali kuwa, hatua hiyo itakuja kuleta hatari kubwa kwa Taifa. `Mimi nasema `No`, tutaimaliza nchi sasa , eti makontena yao yakiingizwa nchini, yanapita bila kukaguliwa? Hapana, hii ni hatari. Serikali inapaswa kuliangalia upya suala hili,` aliongeza Bibi Anne Kilango Malecela ambaye pia ni mfanyabiashara. Naye Bi. Joyce Machimu (CCM-Viti Maalum), aliitahadharisha serikali kuhusu huo mpango wa kutokagua baadhi ya bidhaa za wafanyabiashara, kwa maelezo kuwa, wafanyabiashara wengine wasiokuwa waaminifu, wanaweza kutumia mwanya huo kuingiza mihadarati nchini.
SOURCE: Nipashe






3) nitumie email yako, nikutumie kiambatanisho cha kurasa tisa cha mtandao wa walaji wakuu bongo ambayo ina-link na hizo habari hapo juu.