Friday 23 February 2007

THE TRUTH AT LAST!

Revealed: How British bosses bribed foreign governments to buy military Land Rovers in the 1970s- and how the two-faced British Government covered up the truth.

In May 1977 the Daily Mail newspaper ran a sensational front-page story revealing how the former British Leyland had set up a slush fund to bribe foreign governments into buying Land Rovers.
It was a story that threatened to bring down the Callaghan Labour Government, which went to great lengths to discredit the story-and ultimately won.
The newspaper was eventually forced into humiliating climbdown and subsequently paid out massives damages to the BL executives named and shamed in the original report.
But now LRO can reveal that the original story was accurate all along-and the the Prime Minister of that day, Jim Callaghan, and his chancellor of the Exchequer, Denis Healey, were well aware of the facts.
But instead of telling the truth and vindicating the journalists behind the expose, they turned their backs as the nationalise motor giant`s crooked directors sued for damages.
BL`s chairman, Lord Ryder received £40,000 in damages(the equivalent of £200,000 today). Fellow directors Alex Park and David Andrews, as well as the Government`s Industry Secretary, Eric Varley, also received undisclosed but substantial sums.
But 29 years on, top-secret Government documents from the time are now in the public domain and reveal that the Daily Mail`s original story was in fact true.
The Cabinet was aware that Bl had set up an offshore fund, from which it made clandestine pay-offs of £4.2 million(£20 million today) to bribe decision makers in Middle East and Afrcan countries.
Evidence revealed this month includes £700,000 paid into the bank aacount ot the brother-in-law of the man in charge of buying vehicles for Saudi Arabian army - who worth of subsequently bought £5 million worth of military Series III Land Rovers.
Many of the Men right in the heart of the scandal - including Callaghan, Lord Ryder and wrongly discredited Daily Mail editor Sir David English - are now dead.
But the former Chancellor Healey makes no secret of the cover-up at the time, admitting:'It would have do more harm than good to tell the truth'.
The Daily Mail says his response 'stinks'
'This sorry saga is a parable of how vital it is to have a free Press - and the miserable lenghts to which politicians will go to suppress that freedom,' they comment.

"story told by LANDROVER OWNER INTERANTIONAL MAGAZINES"

Monday 19 February 2007

LandRover-Dominant Military Vehicles!

Je wajua siri ya Gari aina ya Landrover kuwa ndiyo magari yanayotumika zaidi Jeshini duniani kote? Pata habari zaidi kupitia blogu hii hivi karibuni.

Barua ya wazi kwa Mh.Rais Jakaya Mrisho Kikwete




Mh. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete, ifuatayo ni barua ya wazi kwako kuelezea hali halisi ya wanyama pori katika baadhi ya mbuga zetu za wanyama nchini Tanzania. Swala hili lilikuwa liwasilishwe kwako siku ulipokutana na watanzania waishio nchini Uingereza katika kipindi cha maswali na majibu, lakini kutoka na uhaba wa muda haikuwezekana hivyo basi kutokana na maendeleo ya sayansi na tekinolojia ya dunia ya sasa imefikirika labda kwa njia hii bado itasaidia kufikisha ujumbe huu kwako.

Mh. Rais, itakumbukwa kwamba hivi karibuni Tanzania imetangazwa kuwa ni nchi moja wapo katika zile nchi zenye rekodi ya kuwa na Maajabu Saba ya Dunia(Seven Wonders of The World) kutokana na uhamaji wa mamilioni ya wanyama aina ya nyumbu(kama sijakosea) kila mwaka toka mbuga za Serengeti wakivuka mto Mara na kurudi tena kutokana na tofauti ya vipindi vya majira ya hali ya hewa, ama kwa hakika jambo hili ni la kihistoria na ni jambo la kujivunia mno.
Lakini si hilo tu kwani pia unapoongelea bara la Afrika, ukitazama ramani(Atlasi) ya Dunia, nomino/jina Tanzania si geni kabisa katika kuelezea vielelezo kadha wa kadha juu ya la Bara hili, kwa mfano unapoongelea sehemu ya juu kabisa ya mwinuko(highest peak) katika bara zima la Afrika ni lazima uitaje Tanzania, kwa maana mlima wa Kilimanjaro ndiyo mlima mrefu kuliko yote barani Afrika, tena unapotaka kuongelea kina kirefu zaidi barani Afrika utaongelea ziwa Tanganyika ambalo limepitiwa na bonde la Ufa(Rift Valley) hivyo basi ni lazima uitaje nchi ya Tanzania ambayo kwayo ziwa Tanganyika ndiyo kiini cha jina Tanzania. Unapokuja kuongelea ziwa kubwa kuliko yote barani Afrika yaani ziwa Victoria, ni wazi kwamba utakuwa unaikosea Tanzania usipoitaja kwa maana sehemu kubwa ya ziwa hili iko upande wa Tanzania tukushiriki pamoja na majirani zetu nchi za Kenya na Uganda na bila kusahau pia kwamba hapo awali chanzo cha mto Nile ambao ni mto mrefu kuliko yote barani Afrika, kilijulikana kuwa ni ziwa Victoria, Victoria = Tanzania, ambavyo ni tofauti hivi sasa.
Licha ya yote hayo Tanzania inajulikana kuwa na madini yapatikanayo nchini Tanzania pekee si kwa Afrika tu bali Duniani kote, madini ya TANZANITE.
Na kwa kumbukumbu za kihistoria itakumbukwa kwamba fuvu la kichwa cha mtu ambaye anasemekana alikuwa wa kwanza kuishi Duniani lilipatikana Tanzania, fuvu la "Zinjanithropas",sina hakika wanasayansi wameshagundua lipi kwa sasa.
Kwa kifupi ni kwamba Tanzania imekuwa kwenye ramani ya Dunia na katika Historia kwa muda mrefu sasa, ingawaje utangazwaji wake umekuwa hafifu.

Miaka ya hivi karibuni ambapo Tanzania imekuwa ikiianza kujitangaza kwa kasi mpya,nguvu mpya na ari mpya hasa kupitia swala la utarii, ieleweke wazi kwamba majivuno haya huenda yakawa ni ya muda mfupi tu pengine kipindi cha miaka kumi(10) mpaka labda ishirini(20) hivi. Hii ni kutokana na hali ilivyo huko mbugani.

Mh. Rais, ukweli ni kwamba hali halisi ya Uvunaji wa Wanyama Pori katika mbuga zetu unafanyika kiholela sana na kama hali hii itaendelea hivi tusijepigwa na bumbuwazi katika kipindi cha miaka iliyoelezewa hapo juu baadhi ya wanyama katika mbuga zetu wakawa wametoweka kabisa, mbaya zaidi baadhi ya wanyama hao huwenda ikawa na ile ya wanyama ambao wamekuwa ni kivutio zaidi, wanyama ambao wamewekwa kwenye orodha iliyopewa jina la "The Big Five", mfano wanyama kama Simba(mfalme wa Nyika), ambapo wanyama kama hawa wanapatikana kwenye nchi chache Afrika moja wapo ikiwa ni Tanzania.
Huvunaji huu wa wanyama wa kiholela ambao unaendana na uchukuzi wa takwimu za idadi ya wanyama kiholela yaani kwa makisio ama makadirio tu ambao sio sahihi unaoambatana na rushwa iliyokithiri, ukiendelea kufumbiwa macho ama usipovaliwa njuga itabaki kuwa historia kwa vizazi vijavyo kwamba Tanzania ilikuwa na hiki na kile na pengne watoto wetu na wajukuu itawapasa kwenda nchi nyingine kuona yale tuliokuwa tunajivunia nayo watanzania tena kwa gharama kubwa mno na wengine kushindwa kufanya hivyo kabisa.

Mh. Rais ni haya machache tu ambayo ningependa kuwasilisha kwako!

Wako mtiifu katika Ujenzi wa Taifa la Tanzania

Mtanzania Mzalendo!

Sunday 18 February 2007

Mh. J.K atizimiza ahadi- London

Kama alivyoahidi hapo awali alipokutana na Watanzania waishio Uingereza mwezi wa Januari 2007, Mh. Rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete, jana tarehe 17 Februari 2007 alikutana tena na wananchi wake hao kwa kipindi cha maswali na majibu. Wananchi hao ambao walikuwa wakiisubiri kwa hamu siku hii, walijitokeza kwa wingi ukumbini hapo, kwa wale waliofikiri pengine ahadi hii iliyotelewa hapo awali ilikuwa ni propaganda tu za mambo ya kisiasa, waswahili wanasema,"wameula wa chuya kwa uvivu......."

Kipindi cha maswali na majibu kilifunguliwa rasmi pale tu Mh. Rais alipokabidhiwa ukumbi na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mama Maajar, naye Mh. JK bila ya kupoteza muda alitoa ruksa kwa wantanzania kuanza kuuliza mwaswali moja kwa moja. Kwa kuwa hapakuwepo na mpango maalum wa uulizaji Mh. Rais alichukua jukumu la kuwa mwenyekiti na kuanza kupokea maswali moja kwa moja kutoka kwa wananchi wasiopungua kumi na wawili kwa mkupuo mmoja na kuyajibu moja baada ya jingine, ambapo alifanikiwa kujibu maswali yote zaidi ya ishirini na manne yaliyouulizwa na wananchi wake.

Swala ambalo tunaweza kusema lilikuwa ni gumzo ama kuchukua sehemu kubwa na majadiliano lilikuwa ni swala la Utanzania yaani uzawa ama tuseme baadhi ya wananchi wengi ambao wengine tayari wamekuwa na uraia wa Uingereza ama bado wanasubiri na hawajui hatima yao ni nini wamekuwa na hamu kubwa sana ya kujua swala la uraia wa nchi mbili limefikia wapi. Katika hao aliyekuwa kivutio zaidi cha siku ni mzee mmoja ambaye aliingia nchini katika nchi ya Malkia tangu mwaka wa 1957.

Mtazamo/ Mawazo Binafsi!
Ushauri wangu ni kwamba kutokana na hali ya maendeleo ya tekinolojia na kwamba hizi ni zama za habari(Information Age), ninafikiri kwamba Mh. Rais anapojiandaa kukutuna na watanzania wake sehemu ambazo hajatembelea ama akiwa na nafasi ya kutembelea hata zile sehemu ambazo tayari ameshazitembelea basi ujio wake unapoweka wazi siku kadhaa kabla ya uwepo wake katika maeneo husika kuwepo na mpango wa wananchi kuutuma/kuulizwa maswali au maoni yao kwa njia ya mtandao aidha barua pepe, ama tovuti maalum ili kusudi siku rasmi ya kukutana Mh. aweze kujibu tu maswali moja kwa moja kwa kwa kunukuu kutoka hizo barua pepe, hii pia itasaidia Mh. kuwa na majibu kamili na ya kiutalaamu kwa kila swali kwa maana tayari hatakuwa ameshaulizi habari(information) kamili toka kwa wizara husika au wanaohusika hivyo kurahisisha zoezi hili, kuokoa muda na kuongeza uzalishaji. Kwa muda ule mchache wa masaa mawii matatu ambao unakuwepo wa maongezi kidogo basi yanaweza kujibiwa baadhi ya maswali ya papo kwa papo.

Ushauri kwa Mh. Rais na Viongozi Wengine.
Ushauri wangu kwa Mh. rais na viongozi wengine ni kwamba,nawaomba muwe wapenzi wa kutembelea vyombo mbali mbali vya habari, ambavyo kwa sasa si televisheni na magazeti pekee kama ilivyokuwa zama hizo, ambavyo vingine vimekuwa vikitumika kupotosha ukweli wa habari kwa muda mrefu sasa, kwa sasa mnaweza kupitia tovuti,blogu binafsi mbali mbali
zenye habari nyeti kuliko hata ambavyo mnaweza kufikiri. Hizi ni zama za Utandawazi na mambo mengi yako bayana na yataendelea kuwa bayana siku hadi siku kwa maana kila mtu sasa ana uwezo wa kuwa mwanahabari na kurusha habari hewani duniani kote bila ya kutegemea vyombo kama BBC, CNN, Radio Tanzania, TVT ama ITV na vingine vingi na pengine bila hata malipo kama ambavyo nifanyavyo mimi na wanablogu wengine wengi tu duniani. Internet ndiyo kila kitu Zama Hizi za Habari kwani hata nanyi pia mnawezakuwa na blogu zenu binafsi nasi tuwe tunazitembelea! Hii ndiyo Dunia ya sasa!

Kwa habari zaidi na picha za tukio hili tembelea tanzaniaone.net, tanzaniaone.com, tzuk.net na tzuk.com.

Endelea kutembelea blogu hii kusoma barua ya wazi kwa Mh. Rais Jakaya Mrisho Kikwete juu ya sakata la Hali Halisi Ya Wanyama Pori huko mbugani.