Monday 12 March 2007

Uhamiaji/Immigration-UK VISA!

Kwa wale wenzangu na mimi ambao tunaendelea kujikita kwa Bibi(Malkia Elizabeti) kwa kujikimu wenyewe na kutegemea kubeba box ama kuishi kiujanja ujanja, hali imeendelea kuwa ngumu kwa sasa!
Ni wazi kwamba kwa mtanzania ama mgeni(foreigner) kutoka nchi zetu za Dunia ya tatu ambaye yuko nchini Uingereza katika miaka hii ya karibuni( "Msomi bila kusoma ama Mkimbizi bila Vita")-according 2 MrII a.k.a SUGU, hali si kama ilivyokuwa miaka 4,5,6,10 iliyopita. serikali ya Bi Mkubwa(Malkia) imeendelea kubana na kuonyesha kuchoshwa na wageni.
Kuna habari kwamba hivi karibuni serikali hii itakuwa inatumia ujumbe wa simu za mkononi sms/txt msg kuwataarifu watu ambao visa zao zinaelekea kwisha ya kwamba wajiandae kuondoka nchini kwa hiari kabla sheria haijachukua mkondo wake. Si hivyo tu bali pia jumbe hizi za sms/txt zitatumwa pia kwa wenye nyumba(Landlords/LandLadies) kuwataarifu kuwa wateja/wapangaji wao muda wa kuishi hapa umekwisha na kwamba Landlord/Landlady atakayekiuka kushirikiana na serikali kuwafichua watu hawa atalipa faini kwa kila kichwa ambayo inaweza kuwa ni zaidi ya ile wanayolipa waajiri walioajiri wafanyakazi bila makaratasi ambayo ni paundi za mwingereza elfu tano(£5,000) zaidi ya milioni kumi(10,000,000/-) fedha za madafu kwa kichwa na zaidi.
Kwa mtaji huu tuendelee kujetemgemea mtiririko wa vijana nyumbani katika miaka 2 ijayo! Swala ni kwamba je, Vijana tumejiandaaje na Wimbi hili?
Wazaramo wanasema, "We kalaga bao miangu na kidonda chako kuku wakidonole"

No comments: