Thursday 28 December 2006

Watanzania Waishio Uingereza!

Watanzania waishio nchini Uingereza wameshauriwa kurudi nyumbani Tanzania kuisadia serikali ya awamu ya nne kuendelza nchini. Maneno hayo yalisemwa na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mama Maajar.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mama Maajar amewashauri watanzania wasomi waishio Uingereza kurudi nyumbani kusaidia kuleta maendeleo ya nchi badala ya kubakia kuilalamikia serikali kila mara juu ya hili na lile. Mama Maajar aliyasema hayo alipokutana na watanzania jijini London kuwasalimia na kujitambulisha kwao wiki chache zilizopita. Mama Maajar aliwataka watanzania hao wajiulize ni nini wataifanyia nchi yao na si nchi itawafanyia nini!

Takwimu zinaonyesha kwamba katika wantanzania elfu tano(5,000) wasomi waishio Uingereza ni asilimia tano (5%) tu kati ya hao wanaofanya kazi zinazoendana na taaluma zao na waliobaki yaani asilimia tisini na tano (95%) hufanya vibarua tu (unskilled labour) ili kuweza kusukumana na hali ngumu ya maisha hapa nchini Uingereza.

Katika kipindi cha miaka mitano hadi kumi iliyopita watanzania wengi waliongia nchini Uingereza aidha kwa ajili ya kujiendeleza kimasomo, matembezi ama kikazi walitawaliwa na mawazo duni kwamba wamefika peponi na mawazo ya kurudi Tanzania kwao ilikuwa ni ndoto. Huu tunaweza kuuita ni ulimbukeni. Lakini hali ni tofauti kwa miaka ya sasa ambapo wimbi la watanzania kurudi nyumbani tanzania limeongezeka mno. Hali hii inaweza kuwa ni kutokana na kasi ya maendeleo kidunia, lakini pia tatizo kubwa limekuwa ni swala zima la muungano wa nchi za ulaya. Mmiminiko wa waulaya mashariki nchini Uingereza umeleta mfakarakano mkubwa sana na ongezeko la ugumu wa maisha.

Kwa wale ambao bado hawajajiwekea mipango madhubuti ya kujiandaa kurudi nyumbani katika kipindi cha miaka miwili mitatu ijayo wakifiri kwamba hapa ndiyo nyumbani ni wazi kwamba wanajidanganya nafsi zao.

Wazaramo wanasema ,"Ukae kunoga"

No comments: