Thursday 18 January 2007

CCM London wakutana na M/Kiti Taifa CCM

Wanachama wapya na wale wa zamani wa CCM tawi la London wakutana na M/kiti Taifa Mh. J.K. Halfa hiyo iliyofanyika katika Hotel aliyofikia Mh.Rais ambapo ndipo Mh. alikutana na watanzania waishio UK siku ya jumapili ya tarehe 14 Jan 2007, ni Hoteel ya Churchill katikati ya mji wa London.

Hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na wana CCM-London, ilifunguliwa na Katibu wa Muda wa Tawi hilo ndugu Mpopo ambaye alimkaribisha M/kiti wa muda wa tawi Nd. Sharif Maajar ambaye alisoma risala fupi kwa Mh. Rais. Naye Mh.Rais ambaye ndiye m/kiti taifa CCM aliongea machache na kuwashukuru wale wote walijitolea kufanya shughuli hii na hali sema kwamba kabla ya kuwepo kwa vyama vingi kulikuwako na ofisi za CCM katika kila Balozi lakini baada ya kuingia kwa utawala wa vyama vingi ndipo serikali ilipoona ni vema kuacha balozi kubakia shughuli za kiserkali pekee, kwa hiyo amefurahishwa kuona wana CCM wa London wametafuta jinsi ya kukutana pamoja na kwamba CCM taifa itakuwa itashirikiana na tawi hili na kuleta taarifa za mara kwa mara ya yale yote yanayoendelea taifani.

Shughuli hii ilihudhuriwa na baadhi ya mawaziri, wabunge, Balozi, wafadhili "Malinzi family", Naibu Meya wa Jimbo la Ilala, waandishi wa habari na wanachama kutoka pande kadhaa za UK ambao baadaya Mh.Rais kuaga akiwa tayari kuelkea Tanzania kuhudhuria mazungumzo katika ya CCM na CUF, wao walienda na shuhguli ya kuchukua kadi zao za chama. Taarifa iliyosomwa na m/kiti wa tawi imeeleza kuwa mpaka sasa tawi hili lina wajumbe waliokwisha jiandikisha zaidi ya themanini(80) na kati ya hao walikwisha lipia kadi zao ni arobaini na mbili(42), kumi(10) wakiwa ni wanawake. Kadi inauzwa paundi tatu(£3) za mwingereza na ada ya uanachama ni paundi moja(£1) ya mwingereza kwa kila mwezi.

No comments: